September 11, 2015

UWANJA WA NYAMAGANA KWA SASA...

Licha ya Uwanja wa Nyamagana uliopo Mwanza kuwa wa kwanza kufanyiwa marekebisho ikiwemo kutakiwa kuwekewa nyasi bandia, wakazi wa jiji hilo wamelalamika kukwama kwa mchakato huo na badala yake, Uwanja wa Kaitaba uliopo mkoani Kagera kuwa kwenye hatua za mwisho za marekebisho ikiwemo kuwekewa nyasi bandia.


Wakizungumza na gazeti hili, baadhi ya wadau wa mchezo wa soka, wamelilalamikia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana na hali hiyo wakidai limeutelekeza Uwanja wa Nyamagana huku ule wa Kaitaba ukipewa kipaumbele.

Akizungumza juu ya maendeleo ya Uwanja wa Kaitaba, Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Kagera (KRFA), Salum Chama aliliambia gazeti hili kuwa ndani ya wiki tatu zijazo wanatarajiwa kuona uwanja wao ukiwekewa nyasi bandia baada ya marekebisho mengine kukamilika.
 
MALINZI (WA NNE KUSHOTO) AKIKAGUA UWANJA WA KAITABA...
“Nyasi zitawekwa hivi karibuni,” alisema kiongozi huyo ambaye chama chake kinaongozwa na mwenyekiti Jamal Malinzi ambaye pia ni rais wa TFF.

Kuhusu nyasi bandia, Chama alisema: “Aliyepewa tenda ya kutengeneza uwanja ndiye ambaye amejitolea kulipia nyasi bandia kutoka bandari, ndiyo maana zimeshapatikana.”

Akizungumzia kukwama kwa Uwanja wa Nyamagana, Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa, alisema: “Serikali haijatoa msamaha wa kodi katika vifaa vilivyokwama bandarini ikiwemo nyasi bandia. Fifa imetuambia kuwa, ikifika Desemba, mwaka huu kama mambo yatakuwa bado, basi Fifa itazuia miradi yote. Tunasikitika sana kuona serikali imetugeuka na kukataa kutuondolea kodi kwenye vifaa hivyo.”


Licha ya kuanza kufanyiwa marekebisho, Uwanja wa Nyamagana umeanza kuchakaa kwa kuwa matengenezo yamesimama na hakuna kinachoendelea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic