September 13, 2015


Mshambuliaji Emmanuel Okwi alilazimika kuvunja mkataba na Simba ili aondoke kwenda Ulaya.

Okwi amejiunga na timu ya Sonderjyske inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza baada ya klabu hiyo kuelezwa kulipa dola 110,000 (Sh milioni 220).

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema walimzuia Okwi kuondoka kwa kuwa hakikuwa kipindi kizuri kumuuza, lakini akaamua kuununua mkataba wake.

“Wale jamaa awali walitaka kutoa dola 150,000. Lakini tukakataa, unajua ndiyo tunajenga timu na Okwi alikuwa mchezaji tegemeo. Tukakataa.

“Mwisho Okwi akalazimika kuununua mkataba wake kama kipengele kimoja ndani ya mkataba kinavyoeleza.
“Kipengele kinaeleza atoe dola 100,000.

"Akawa ametushinda hata hivyo tukaingia kwenye makubaliano upya na kufanikiwa kuongezewa anagalau dola 10,000,” alifafanua Hans Poppe.


Hans Poppe alikuwa akielezea kwamba hawakuwa tayari Okwi aondoke, lakini mkataba ukawabana. Zaidi soma makala ukuraza wa 12&13.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic