Pamoja na Yanga kushinda mechi tatu mfululizo,
huku mshambuliaji wake Donald Ngoma akifunga kila mechi, Mwenyekiti wa Yanga,
Yusuf Manji amesema Yanga imefanya usajili kama ilivyotaka kwa asilimia 75.
Manji amefanya mahojiano maalum na gazeti hili na
kusema, kwa anavyoona, usajili wa Yanga haujawa asilimia 100 kama ambavyo
aliamini utakuwa.
Yanga tayari imecheza mechi tatu, ikianza
kuitwanga Coastal Union mabao 2-0, ikaikung’uta Prisons 3-0 kabla ya kuiangukia
JKT Ruvu kwa mabao 4-1.
Mwenyekiti huyo kijana wa Yanga amesema, anaamini
usajili wao umefanikiwa kwa asilimia 75 ingawa kwa wachezaji walionao, wanaweza
kuongeza juhudi na kufikia asilimia 100.
“Juhudi za wachezaji walio katika kikosi kwa
sasa, inaweza kufanya usajili ufikie yale malengo ya asilimia mia.
“Kwa sasa naweza kusema bado, ni kama mafanikio
ya asilimia sabini na tano hivi. Kadiri tunavyokwenda na wachezaji na kocha
kama wataongeza juhudi zaidi wakitaka kushinda kila mechi, ninaweza kusema sasa
tumefanikiwa kwa asilimia mia,” alisema Manji.
Manji amesema uongozi wa Yanga umekuwa karibu na
kamati zote pamoja na benchi la ufundi kwa kuwa unataka Yanga inayofanya vizuri
kitaifa na kimataifa.
“Tumekuwa tukifanya vizuri nyumbani, vizuri
tukifanya vizuri kimataifa. Ni jukumu la wachezaji kupambana, nasi tuko pamoja
nao,” alisema.
Yanga ndiyo mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara na
tayari wana mabao nane katika mechi tatu, Ngoma akiwa amefunga matatu.
Tangu Manji amechukua nafasi ya mwenyekiti, Yanga
imekuwa ikishika nafasi ya kwanza, yaani bingwa au ya pili na zote imekuwa
ikipata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa.
SOURCE: CHAMPIONI
SOURCE: CHAMPIONI







0 COMMENTS:
Post a Comment