| RUVU SHOOTING KABLA YA KUTEREMKA DARAJA... |
Timu ya Ruvu Shooting inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, imeanza
vibaya harakati zake za kurudi ligi kuu baada ya kuchapwa bao 1-0 na maafande
wenzao wa JKT Mlale ya Ruvuma katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Majimaji
Songea.
Kichapo hicho kimetia doa mipango ya timu hiyo ambayo ipo kwenye
mikakati mizito ya kurudi ligi kuu msimu ujao baada ya msimu uliopita kuporomoka.
Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, alisema licha ya kipigo
hicho ambacho amekiita cha kushtukiza, kamwe hawatavunjika moyo kwani ni mapema
mno.
“Tumekubali tumefungwa
lakini ari yetu ya kucheza ligi kuu msimu ujao ipo palepale, tutajipanga kwa
mechi zijazo ili kuhakikisha tunatimiza azma yetu tuliyojiwekea,” alisema
Masau.
MATOKEO MENGINE: Friends Rengers 1-1
Polisi Dar, Mbao Fc 2-2 Geita Gold Sports, Polisi Morogoro 1-0 Bukina Faso,
Panone 4-0 Oljoro na Lipuli 2-0 Kimondo FC.







0 COMMENTS:
Post a Comment