September 11, 2015

MAREHEMU AKIWA NA MJUKUU WAKE, ANDY AMBAYE NI MTOTO WA KWANZA WA MOLANDI.
Mwandishi mwandamizi wa gazeti la Championi, Wilbert Molandi amepata msiba mkubwa wa kufiwa na baba yake mzazi.


Andrew Molandi amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Mzee Molandi amefariki dunia baada ya kuugua kwa siku kadhaa na mipango ya mazishi inafanywa nyumbani kwake Kigogo jijini Dar es Salaam.

Molandi ameiambia SALEHJEMBE, wako katika hatua za mwisho kuhusiana na maziko ya mzee wake.


“Ndugu tunakutana kwa ajili ya kujadili na baada ya hapo tutatoa taarifa kama mwili utasafirishwa au tutazika hapa Dar es Salaam,” alisema Molandi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic