September 12, 2015


Kocha Mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ametamba kuwa, kama haki itapewa nafasi katika Ligi Kuu Bara, timu yake itafanya maajabu na inaweza kubeba hata ubingwa.

Kihwelo ambaye ni maarufu kama Julio amesema Mwadui FC chini yake ina uwezo mkubwa wa kubeba ubingwa.

“Tofauti na wengi wanavyofikiri, Mwadui inaweza kubeba ubingwa. Kwao ni maajabu lakini kwetu inawezekana.

“Tunachotaka ni haki ifuate mkondo wake, kama itakuwa hivyo tutawashangaza wengi sana,” alisema Julio.

Mwadui FC ambayo imepanda ligi kuu msimu huu, inaanza leo kucheza na Toto African ikiwa ugenini mjini Mwanza.


Msimu uliopita, Mwadui FC ilipanda pia kwa wingi wa pointi, lakini mwishoni Stand United ya Shinyanga pia ikashinda rufaa na kuchukua nafasi ya Mwadui FC.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic