![]() |
| PLUIJM... |
Yanga
kulitetea Kombe inalolishikilia la Ligi Kuu bara kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi
ya Coastal Union.
Yanga
imepata ushindi huo leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam huku mabao
yote yakifungwa katika kipindi cha kwanza.
Simon
Happygod Msuva na Donald Ngoma raia wa Zimbabwe ndiyo waliofunga mabao hayo
mawili ya Yanga.
Ahmed
Shiboli wa Coastal Union alipoteza nafasi tatu safi za kufunga ambazo
zingewasaidia angalau kupata bao la kufutia machozi au kusawazisha zaidi.
Yanga
bao walipoteza nafasi nyingine tatu kupitia Amissi Tambwe, Msuva na Haruna
Niyonzima.
Yanga
ambao ni mabingwa watetezi wanaungana na Simba, Toto African, Majimaji, Azam
FC, Mtibwa Sugar na Kagera Sugar kuwa timu zilizoanza na ushindi katika siku ya
kwanza ya ligi.
Leo
kulikuwa na mechi hiyo moja kati ya Yanga dhidi ya Coastal Union wakati pazia
la ligi hiyo lilifunguliwa jana kwa mechi saba kuchezwa.
MECHI ZA JANA:
African
Sports 0-1 Simba
Majimaji
1-0 JKT Ruvu
Azam
FC 2-1 Prisons
Stand
Utd 0-1 Mtibwa
Toto
1-0 Mwadui
Mbeya
City 0-1 Kagera








0 COMMENTS:
Post a Comment