September 13, 2015


Uhuru Selemani ameanza kazi nchini Afrika Kusini wakati timu yake ya Royal Eagle ikiichapa Amazelu kwa mabao 2-1.


Raha zaidi, ikiwa ndiyo mechi yake ya kwanza, Uhuru amefanikiwa kufunga bao la ushindi.

“Nina furaha sana, ni mechi ya kwanza ya ligi, nimefanikiwa kufunga bao la ushindi,” alisema Uhuru alipozungumza na SALEHJEMBE.

Kabla ya hapo, Uhuru hakucheza mechi takribani tatu kutokana na kutokuwa amepata kibali cha kufanya kazi.


Mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba, amesajiliwa na Jomo Cosmos kabla ya kupelekwa kwa mkopo Royal Eagles yenye makao yake makuu jijini Durban.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic