October 10, 2015




Baada ya uficho wa siku kadhaa, sasa mambo hadharani kuwa Kocha Juma Mwambusi, amechukua nafasi ya Charles Boniface Mkwasa.


Mwambusi aliyekuwa Kocha wa Mbeya City, amechukua nafasi ya kocha msaidizi wa Yanga iliyoachwa na Mkwasa ambaye sasa ni Kocha Mkuu wa Taifa Stars.

Mwambusi tayari amewaaga Mbeya City na rasmi amesajiunga na Yanga kwa mkataba wa  miaka miwili, huku akitarajia kutambulishwa kesho.


Kocha huyo ataanza kazi rasmi keshokutwa Jumatatu chini ya Kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic