October 1, 2015


Wanasimba wenzangu kwanza tumshukuru muumba kwa uwezo wake kutuwezesha kumaliza salama mechi yetu ya dhidi ya Stand United ya Shinyanga.


Na kwa pekee tumshukuru yeye kwa kutujaalia kupata ushindi katika game hiyo iliyokuwa ngumu.

Pia nichukue fursa hii kuwapongeza wachezaji wetu na bench Ia ufundi kwa kuweza kupambana na hatimaye kuzoa points zote tatu hii.

Hakika tulikuwa na mshindani halisi wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Nakiri wazi kabisa Stand United ni timu nzuri sana na wanastahili pongezi.

Na kama ilivyo ada shukran makhsusi ziwaendee mashabiki wetu kwa kuishangilia timu yao kwa nguvu sana na kwa wale ambao hawakuja leo uwanjani. Tunajua dua na sala zenu mlizielekeza Uwanja wa Taifa.

Ligi bado mbichi sana. Tusahau sasa machungu yetu ya kupoteza mechi dhidi ya watani. Maisha lazima yasonge mbele na sote tupeleke akili yetu kwenye game za mkoani Mbeya ambazo tunaujua ugumu wake.

AHSANTEN washabiki wa Simba.

Mungu ibariki Simba
Reclaiming our glory


Simba Nguvu Moja

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic