November 14, 2015

MPIRA UMEKWISHAAAAAAA
Dakika 3 za nyongezaDk 84, Ulimwengu anawatoka mabeki watatu wa Algeria lakini wanawahi na kuutoa na kuwa kona ambayo hata hivyo haizai matunda

KADI Dk 81, Bentaleb analambwa kadi ya njano kwa kumwangusha Ngassa kwa makusudi
KADI Dk 80 Himid Mao analambwa kadi ya njano kwa faulo, hii ni kadi ya kwanza katika mechi hii

Dk 79, Kapombe anapiga krosi nzuri kabisa na mpira unamkuta Ulimwengu anapiga kichwa, unatoka pembeni kwa lango la Algeria

Dk 74 Slimani tena anaifungia Algeria bao la pili baada ya kumchambua BArthez na kufunga bao

Dk 74, Samatta anapiga shuti kali lakini kipa anadaka vizuri
GOOOOO Dk 71, Islami Slimani anaipatia Algeria bao kwa ulaini kabisa
Dk 69 Farid anawatoka mabeki wawili wa Algeria lakini wanaokoa na kuwa kona ambayo inachongwa na Himid Mao, lakini haina madhara sana

Dk 68, Bentaleb anampiga chenga Kapombe, anapiga shuti juu kama anatungua minazi

SUB Dk 63 Stars wanaimuingiza Mrisho Ngassa kuchukua nafasi ya MAguri na Saidi Hamisi Ndemla anaingia kuchukua nafasi ya Mudathir. Hata hivyo inaonekana kama Mkwasa amefanya mabadiliko yanayoonyesha anaamini ushindi umepatikana. Vema angeingiza mtu wa kukaba zaidi

Dk 60 hadi 63, mpira unaonekana kuchezwa katikati zaidi huku Algeria wakiendelea kupoza mpira na kupiga pasi za kupenyeza ambazo ni hatari kwa Stars

Dk 59, Ulimwengu anapiga krosi safi lakini sentimeta chache kabla haujamfikia Samatta beki anaokoa na kuwa kona ambayo inapigwa na Himid Mao lakini haina madhara

Dk 55, Samatta anaingia tena ndani ya eneo la hatari na kupiga shuti lakini kipa anadaka vizuri kabisa

GOOOOOOOOOO Dk 54, Samatta anawachambua mabeki wa ALgeria kama karanga na kufunga bao safi kabisa nje ya 18
Dk 53, Farid anapokea pasi nzuri ya Samatta anapiga krosi lakini Ulimwengu anashindwa kuuwahi
na Dk 52, Ulimwengu anaukatiza msitu wa mabeki wa Algeria lakini mpira unamzidi kasi
Dk 49, Algeria wanapata mkwaju wa adhabu nje ya eneo la 18 la Stars, wanapiga adhabu hiyo lakini mpira unatoka nje

Dk 48, Stars wanaonekana kupoteza ile nidhamu ya kipindi cha kwanza katika ukabaji ambayo ni hatari kwa upande wao. Bentaleb ni hatari lazima wawe makini
Dk 47 Bentaleb anatoa pasi nzuri inayosababisha kona baada ya Haji Mwinyi kuokoa, lakini kona haina madhara


Dk 46, Algeria wanamtoa Bnfodil Isha wanamuingiza Bentaleb, kiungo hatari anayeichezea Tottenham ya England


UMILIKI WA MPIRA
STARS 53% ALGERIA 47%
MASHUTI 
STARS 6 ALGERIA 1
MAPUMZIKODk 45+1
Dk 45, Algeria wanaonekana kuamka na kutaka kuanza kushambulia hata hivyo Stars wanaonekana kuwa makini na kuokoa

GOOOOOOOOO Dk 43 Elius Maguri anafunga bao la kichwa baada ya kuiwahi krosi safi ya Haji Mwinyi Mgwali aliyegongea vizuri na kinda Farid Mussa

Dk 39, Samatta anapokea pasi ya Farid, yeye akiwa na kipa anashindwa kufunga....
Dk 35, Farid anaingia vizuri ndani ya eneo la hatari, yeye na kipa anapiga mpira unatoka sentimeta moja pembeni ya lango la Algeria

Dk 34 Stars inapata kona ya pili, inachongwa vizuri Algeria wanaokoa na kuzaa kona ya tatu, anapiga Mao Himid lakini Algeria wanaokoa
Dk 31, Kapombe anapiga shuti kali lakini lipatita juuu
Dk 28 Samatta anaingia katika eneo la hatari, anamvuka kipa na kupiga shuti lakini beki anawahi kabla halijavuka msitari
 Dk 21, Samatta anapata pasi nzuri ya kisigino, anaingia na kupiga shuti kali linagonga mwamba wa juu au mtambaa wa panya na kutoka nje

Dk 19, kapombe anapiga mpira mzuri wa adhabu unaingia katika eneo la lango la Algeria, mpira unamkuta MUdathir naye anapiga shuti kuuuubwaaaaaaaa

Dk 17, bado Algeria wanaonekana kutumia zaidi mbinu ya kupoteza muda ambayo kwa kiasi fulani wanaweza kufanikiwa kwani wanapunguza kasi ya Stars ambayo walianza nayo

Dk 13 hadi 15, wachezaji wa Stars wananaswa na mtego wa kuotoa wa Algeria. 

Dk 11 na 12, Waalgeria wanaonekana kupoteza muda kwa makusudi na inaonekana waamuzi bado hawajagundua ujanja wao

Dk 10 Ahmed anaingia vizuri katikati ya lango la Stars lakini anapiga dhuti mtoto, Barthez anadaka kama uji
Dk 8, Ulimwengu anaambaa na mpira kutoka 18 ya Stars hadi 18 ya Algeria lakini anapiga shuti kuuubwaaaaa.

Dk 7, Cannavaro anafanya kazi ya ziada kuokoa, inakuwa kona na Algeria wanapiga haina madhara
Dk 5, Algeria wanaonekana kuanza kucheza taratibu na kuipa wakati mgumu Stars
Dk 3, Samatta anampiga beki chenga na kutoa pasi nzuri kwa Maguri lakini anaugonga mpira mbali na kipa anauwahi

Dk 2 Ulimwengu anatoa pasi nzuri kabisa inayomfikia Mbwana Samatta, yeye na lango anapaisha juuu kabisa
KIKOSI KAMILI HIKI HAPA:
Ally Barthez, Shomari Kapombe, Haji Mwinyi, Kelvin Yondani, Nadir Haroub, Himid Mao, Thomas Ulimwengu, Mudathir Yahya, Elius Maguli, Mbwana Samatta na Farid.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic