Mganda Brian Majegwa sasa ni mali ya Simba na
atakuwa katika kikosi cha Wekundu wa Msimbazi.
Simba imefikia makubaliano na Azam FC ili
kumtwaa Majegwa raia wa Uganda, akipige Msimbazi.
Makubaliano hamefikiwa baada ya kikao kizito
kilichofanyika jijini Dar es Salaam jioni hii na Simba na Azam FC kufikia
mwafaka kuhusiana na Majegwa.
Bado kila upande umekuwa ukifanya siri, lakini
taarifa zinaeleza kwamba Mganda huyo ameishapewa taarifa na sasa kinachofuatia
ni kumalizana kwa kila upande kwa vitendo.
Majegwa alirejea nchini na kuomba kufanya
mazoezi na Simba ili kulinda kiwango chake.
Lakini Azam FC ilianza kulalamika kwamba ni
mchezaji wao lakini bado Majengwa aliweka msimamo kwamba angependa kucheza
Simba na Azam FC wamwache.
0 COMMENTS:
Post a Comment