Kiungo Andrey Coutinho yuko jijini Dar es
Salaam, lakini uongozi wa Yanga, umepitisha uamuzi wa kumtema.
Uamuzi wa Yanga umepitishwa baada ya
majadiliano kati ya uongozi na benchi la ufundi kukubaliana.
Habari zinaeleza Yanga iko katika hatua za
kufikia makubaliano na Coutinho ili kuvunja mkataba wake.
Kocha Hans van der Pluijm ameridhia kuachana na
Coutinho kwa kuwa amekuwa hana msaada wa kutosha.
Lakini Yanga kwa sasa inafanya mchakato huo,
kama pande mbili zitashindwa kufikia mwafaka, basi raia huyo wa Brazil
ataendelea kubaki Yanga hadi mkataba wake utakapokwisha.
0 COMMENTS:
Post a Comment