TP Mazembe ndiyo
wawakilishi wa Afrika katika michuano ya ubingwa wa dunia upande wa klabu.
Michuano hiyo inaanza
Desemba 10 na TP Mazembe inatakiwa kucheza mechi tatu kabla ya kufika fainali.
Desemba 10 itacheza
Auckland City, ikishinda itakutana na timu nyingine iliyovuka na kama itashinda
tena itaingia nusu fainali.
Mechi ya nusu fainali
itakutana kati ya timu ambayo haijajulikana au River Plate ya Argentina na
wakishinda hiyo basi ni fainali.
Lionel Messi atakuwa na
Barcelona ambayo inaanzia moja kwa moja hatua ya nusu fainali kwa kucheza na
mshindi kati ya America dhidi ya Guangzhou Evergrande ya China.
Iwapo Mazembe itashinda
mechi hizo tatu, Barcelona ikashinda hiyo moja, basi nyota zaidi katika timu
zitakazocheza fainali itakuwa ni Messi na Samatta kutoka Tanzania.
Hata hivyo Mazembe wanalazimika
kufanya kazi ya ziada kuhakikisha wanashinda mechi hizo tatu kabla ya kuikamata
Barcelona.
0 COMMENTS:
Post a Comment