January 27, 2016


Licha ya wanachama wa Yanga kufurahia kurejea kwa fundi wa pasi kikosini hapo, Haruna Niyonzima baada ya kumaliza matatizo yake na klabu hiyo, kocha mkuu wa timu hiyo Hans van Der Pluijm amesema bado siyo yule Niyonzima anayemjua.

Kiungo huyo amerejea kikosini wiki iliyopita baada ya kukaa nje tangu Novemba mwaka jana, alipokwenda kwao Rwanda katika majukumu ya timu ya taifa.


Hata hivyo, Pluijm alisema kiungo huyo bado hajawa fiti kwa ajili ya kumtumia, badala yake anatakiwa kuongeza bidii mazoezini ili kurejesha kiwango chake kwani alikuwa nje muda mrefu.

 “Haruna bado hajawa fiti, anatakiwa kujituma zaidi ili kuwa fiti, hata mchezo uliopita (dhidi ya Friends), alikuwa asicheze, lakini  nililazimika kumtumia tu kwa kuwa Makapu (Said) alifiwa na kaka yake na mazishi yalikuwa siku hiyo.


 “Vinginevyo Haruna alitakiwa angalau acheze dakika 20 kwa kuwa hakufanya mazoezi na sisi,” alisema kocha huyo wa zamani wa Berekum Chelsea ya Ghana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic