February 11, 2016


Ujio wa Kocha Jose Mourinho katika klabu ya Manchester United sasa ni gumzo na hofu kuu.

Tayari taarifa zinaeleza kwamba kama Mourinho atatua Manchester United, mara moja atamuuza kiungo Mhispania Juan Mata.

Taarifa zinaeleza Mata aliyenunuliwa na Man United kwa kitita cha pauni million 37 kutoka Chelsea wakati huo Mourinho akiwa kocha, hata Marouane Fellaini aliyenunuliwa kwa pauni million 27 kutoka Everton, naye safari itamkuta.


Mata na Mourinho hawakuwa katika uhusiano mzuri wakati kiungo huyo alipoondoka Chelsea na kujiunga na Man United iliyokuwa ikifundishwa na David Moyes.

Hali hiyo inazidisha hofu, kwamba Mourinho ambaye inaelezwa tayari amekubaliana na Man United kuchukua nafasi ya Louis van Gaal.

Wachezaji hawana uhakika mani atabaki, mani ataondoka wakati kocha huyo atakapotua Old Trafford mwishoni mwa msimu.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic