![]() |
| MGETA (WA PILI KUSHOTO) SIKU ALIPOTAMBULISHA KATIKA KIKOSI HICHO NCHINI UJERUMANI |
Mtanzania Emily Mgeta anayekipiga katika kikosi cha daraja la tano nchini Ujerumani cha Neckarsulm, ameumia.
Mgeta amepata balaa na kuumia nyama za paja pamoja na kifundo cha mguu.
“Kweli niko katika wakati mgumu, nimeumia nyama za paja ambazo daktari amesema zimechanika. Lakini tena niligongwa kifundo cha mguu,” alisema Mgeta alivyozungumza na SALEHJEMBE, yeye akiwa Ujerumani.
Hata hivyo, beki huyo wa zamani wa Simba na Polisi Moro, alisisitiza kuendelea kuvuta subira hadi atajapokuwa fiti.








0 COMMENTS:
Post a Comment