May 16, 2016




Waangola kwa fitna wamo, maana tayari wameanza kuwavuruga Yanga mara tu baada ya kutua kwenye uwanja wao wa ndege wa kimataifa mjijini Luanda.

Mara tu baada ya kutua, Yanga waligundua baadhi ya mizigo ya baadhi ya wachezaji ilikuwa imepotea.
Kazi ya kuanza kuitafuta ikaanza, haikuwa kazi rahisi na kukawa na mzozo mkubwa.

Katika hali ya kawaida ilionekana ni kama njia ya kuwachosha au kuwavuruga mpango ulioandaliwa mapema.

Hata hivyo, ili kuwapa nafasi wachezaji wapumzike walilazimika kuwapandisha ndege nyingine kwenye mji ambao klabu ya Esperanca ilipo ambako ni zaidi ya kilomita 1200 kutoka Luanda.

Yanga ambayo ilianza vizuri mechi yake ya kwanza ya Kombe la Shirikisho kwa kuitwanga Esperanca kwa mabao 2-0 jijini Dar es Salaam, ilitua vizuri katika mji huo.

Lakini baadhi ya mashabiki na viongozi wengine walibaki Luanda wakisubiri ndege nyingine huku wakitafuta mabegi ya wachezaji yaliyopotea.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic