September 23, 2016


Kampuni ya TSN  Kwa kushirikiana na Wasanii wa bongo fleva na bongo Movie wamejitokeza kuwezesha mechi maalum kuchangia wahanga wa Tetemeko la Ardhi lililotokea Bukoba mkoani Kagera.

Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Biashara Jahu Mohamed Kessy, amesema TSN imejitokeza kudhamini mechi hiyo itayofanyika uwanja wa taifa, jumaapili tarehe 25 september, na hivyo kuwataka wananchi, mashirika na kampuni mengine binafsi kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kuchangia na kuwezesha misaada kwa wananchi wa Kagera waliopata maafa kutokana na tetemeko hilo la ardhi.



Alisema wao kama TSN wameguswa na janga hili na hivyo mbali na michango yao mingine ya moja kwa moja wameona umuhimu wa kushirikiana na wasanii wa bongo fleva na bongo movie kuhamasisha uchangiaji huo kwa pamoja ilikuweza kuwashirikisha na wengine.



“TSN, Tanzania sisi Nyumbani, tunaunganisha nguvu ya wasanii hawa kutoka katika tasnia hizi mbili tofauti  kwa lengo la kuhamashisha uchangiaji wa pamoja,”


Alisema mechi hiyo inatazamiwa kuchezwa saa tisa mchana katika uwanja huo wa Taifa jijini Dar es Salaam.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic