October 7, 2016



Stand United jana jioni kwenye Uwanja wa Sokoine imekomaa na kutoka suluhu na Mbeya City huku Toto African ikishinda mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar katika Ligi Kuu Bara. 

Raha ilikuwa kwa kocha mpya wa Toto, Khalfan Ngassa ambaye ni baba mzazi wa kiungo mshambuliaji wa Fanja FC ya Oman, Mrisho Ngassa ambaye amepata ushindi wa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

KHALFAN NGASSA

Mabao ya Toto yalifungwa na Jamal Soud dakika ya 47 na Mohammed Soud dakika ya 80. 

Kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Stand United ya Shinyanga imeonyesha imebadilika msimu huu baada ya kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya wenyeji wake Mbeya City.

Mbeya City sasa imebaki katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 16 moja nyuma ya vinara Simba. Mbeya City imepaa hadi nafasi ya nne na pointi 12.

Stand United imeendeleza rekodi yake ya kutofungwa msimu huu kwani imecheza mechi nane na imeshinda nne na kutoka sare nane.  Mbeya City imecheza mechi nane, imeshinda tatu, sare tatu na kufungwa mbili. 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic