October 18, 2016




Baadhi ya wanachama na mashabiki wa Simba, wakitokea Ngurumo za Simba wametua kwenye mazoezi ya timu yao na kutoa kidogo walichonacho.

Wanachama na mashabiki hao, wametoa katoni kadhaa za maji kwa wachezaji wao waliokuwa wamazoezini wakipambana.

Wamefanya hivyo kwa kuwakabidhi maji hayo viongozi, Katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele na Mussa Hassan Mgosi ambaye ni meneja wa timu hiyo.

Lengo lao lilikuwa ni kuonyesha hamasa na kuwaonyesha wachezaji kuwa wanauwanga mkono na kukubali namna wanavyoifanya kazi yao katika Ligi Kuu Bara hadi sasa. 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic