January 7, 2017



Klabu ya Yanga imekataa kuilipa Simba fidia ya Sh milioni 50 kuhusu ishu ya Hassan Kessy hivyo Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inatarajia kukutana kwa mara nyingine kupitia upya shauri hilo.

Kamati hiyo iliitia hatiani Yanga kwa kosa la kumsajili Kessy ambaye alikuwa akichezea Simba akiwa ndani ya mkataba kwa kutakiwa kulipa fidia ya Sh milioni 50 kwa Wekundu wa Msimbazi.

Akizungumza Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucus alisema: “Tumepokea barua kutoka Yanga ikitaka suala lao lijadiliwe upya, hivyo kamati hiyo inatarajia kukaa wakati wowote kuanzia sasa ili kujadili suala hilo.

“Yanga wamefikisha barua ya kupinga adhabu wanataka hukumu hiyo ipitiwe upya hivyo kamati itakaa wakati wowote kuanzia sasa japokuwa hatujui kama itatenguliwa ama la.”

Aidha, alipotafutwa Katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele kuzungumzia suala hilo, simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu hakujibu.


Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit, naye simu yake iliita bila kupokelewa.

1 COMMENTS:

  1. Maneno ya Kisheria tanatakiwa kuyaangalia kisheria kwa umakini sana, kupitiwa upya kisheria ni REVIEW ambayo haina athari yoyote kwenye maamuzi ya awali, nilidhani YANGA wamekata rufaa (Appeal), na hata uendeshaji na waendeshaji wake kuna namna yake

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic