Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema kikosi cha Simba kitaendelea kuwa pamoja hadi watakaporejea katika Ligi Kuu Bara.
Poppe amesema wameamua kufanya hivyo ili kuhakikisha kikosi chao kinaendelea kuwa pamoja na fiti.
“Uongozi umekubaliana vijana waendelee kuwa pamoja. Tunaona ni sahihi ili kuendelea kuwa vizuri,” alisema.
Alisema Simba itaendelea na maandalizi mfululizo, ikiwezekana kucheza mechi za kirafiki zaidi na zaidi.
0 COMMENTS:
Post a Comment