April 22, 2017


FULL TIME
DAKIKA 3 ZA NYONGEZA
Dk 90, Yanga inaonekana kupunguza kasi baada ya kuona sasa inawzekana kumaliza na ushindi huo na Prisons hawana mipango ya ziada
Dk 86, Mwashiuya anachonga kona nyingine, Msuva peke yake lakini anashindwa kuuwahi mpira
Dk 86, Yanga wanapata kona, Mwashiuya anaichonga, inaokolewa na Mwasote, inakuwa kona tena
SUB Dk 85 anaingia Anthony Matheo kuchukua nafasi ya Tambwe


Dk 80, Martin Emmanuel anaingia kuchukua nafasi ya Chirwa
Dk 79, Mwashiuya anaachia krosi safi kabisa hapa lakini Asukile anaokoa na kuwa kona hapa
Dk 78 Kamusoko anapiga ule mpira wa adhabu lakini unagonga ukuta na kipa anadaka kwa ulaini
Dk 76, kipa wa Prisons anatoka nje ya eneo lake, anacheza mpira na mwamuzi anasema ni faulo
Dk 75 mpira unachezwa zaidi katikati ya uwanja, Yanga wakionekana kupunguza kasi la Prisons wamekosa ubunifu
Dk 70, Chirwa anaingia vizuri katikati ya mabeki wa Prisons wanambana, anaanguka na mwamuzi anasema hakuna faulo
Dk 67, Mwinyi anatengenezewa vziuri kabisa na Kamusoko na kuachia mkwaju mkali kabisa lakini haukulenga lango


Dk 64 Kamusoko akiwa mbali kabisa anajaribu kuachia mkwaju wa mbali lakini unatoka sentimeta chache
Dk 63, MSuva anaachia krosi safi kabisa lakini Prisons wanaokoa na Yanga inapata kona ya nne katika mchezo huu. Inachongwa na Msuva, Priosns wanaokoa tena
Dk 59, Mwinyi, MWashiuya, Kamusoko wanagongeana vizuri kabisa lakini mwisho Msuva anakuwa ameotoa
Dk 56 Hangaya anakwenda kupiga ile penalti, mpira unagonga mwamba na Kamusoko anaosha mbali kabisa
KADI Dk 55 Cannavaro analambwa kadi ya njano kwa faulo hiyo


PENAAAAAAT Dk 55, Meshack Suleiman anaangushwa na Cannavaro na mwamuzi kutoka Tanga anasema ni penaaaaat
SUB Dk 51 kipa Alan Kalambo anaingia kuchukua nafasi ya Ntala upande wa Prisons
SUB Dk 50 Fred Chudu anatoka anaingia Meshack Suleiman upande wa PrisonsDK 48, Asukile anaingia vizuri lakini anashindwa kulenga lango baada ya kuunganisha kona ya Samatta
GOOOOOO Dk 46, Msuva anaachia mkwaju mkali kabisa, moja kwa moja unamzidi Ntala na kujaa wavuni
SUB Dk 45 ameingia kipa Deohratous Munishi Dida kuchukua nafasi ya Kakolanya 


MAPUMZIKO
DAKIKA 3 ZA NYONGEZA
Dk 45 Mwashiuya anafinya vizuri, anaachia shuti hapa, nje
Dk 42, Msuva anapata nafasi nyingine anaachia mkwaju mkali kabisa, unatoka nje kidogo
GOOOOOOOO Dk 40 Chirwa anaunganisha krosi nzuri ya Haji na kuandika bao la pili kwa kichwa
Dk 39, Benjamin Asukile anapiga krosi nzuri kabisa ndani ya lango la Yanga lakini Kakolanya, kipa wa zamani wa Prisons anadaka vizuri kabisa
Dk 37 Prisons wanaonekana kuamka, wanacheza vizuri na kutawala eneo la katikati ya uwanja ingawa bado hawajawa makini katika umaliziaji
Dk 36, krosi safi kabisa hapa ya MWashiuya, Msuva anaruka na kupiga kichwa lakini anapaisha juuu
KADI Dk 33, Kessy naye analambwa kadi ya njano kwa kumlamba mtama Benjamini Asukile


KADI Dk 30, Mohammed Samatta analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Kamusoko aliyemtoka
DK 28, Prisons wanafanya shambulizi jingine, Mwinyi anaondosha na kuwa kona. Inachongwa vizuri hapa lakini Yanga wanaokoa vizuri
Dk 27 kipa wa Yanga, Kakolanya yuko chini pale anatibiwa baada ya kuumia akijaribu kuokoa shuti la Sabianka
Dk 26 Sabianka anaachia mkwaju mkali, unagonga mtambaa wa panya wa lango la Yanga na kurejea uwanjani
Dk 23 Kessy anapanda vizuri akigongeana na Msuva, Tambwe, lakini kipa Prisons anatokea na kunyaka vizuri kama nyani


Dk 21 Krosi nyingine ya Chirwa lakini Tambwe anachelewa kidogo tu, ilikuwa hatari
GOOOOOOOOOOO Dk 15, Tambwe anaunganisha krosi maridadi kwa kichwa na kuandika bao la kwanza kwa Yanga
Dk 8, mpira wa kichwa wa Chirwa unapita juu kidogo tu
Dk 5, bado inaonekana Prisons hawajaamka kwa kuwa Yanga ndiyo wanaopeleka mashambulizi mengi
Dk 1 Yanga ndiyo wameanza kushambulia kwa kasi kubwa wakionekana wanataka bao la mapema


KIKOSI CHA YANGA SC
1. Beno Kakolanya 
2. Hassani Kessy
3. Haji Mwinyi 
4. Kelvin Yondani
5. Nadir Haroub 
6. Juma Makapu
7. Saimoni Msuva
8. Thabani Kamusoko
9. Obrey Chirwa
10. Amisi Tambwe
11. Geofrey Mwashuiya

Benchi:
- Deogratius Munishi
- Oscar Joshua 
- Andrew Vicent 
- Juma Mahadhi
- Antony Matheo
- Yusufu Mhiru

- Emanuel Martin 

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic