April 15, 2017

MAVUGO

Ukiangalia katika mechi tatu za nyuma za Simba za Ligi Kuu Bara, straika Laudit Mavugo hajafunga bao lolote hivyo ametamba kupambana ili afunge bao leo dhidi ya Toto African kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini hapa.

Akizungumza baada ya mazoezi ya jana Ijumaa asubuhi uwanjani hapo, Mavugo raia wa Burundi alisema sasa ni wakati wa kujituma kuliko wakati wowote ndani ya Simba.

“Sasa tuna presha kubwa sana ya ubingwa, huu ni wakati wetu sisi wachezaji hasa washambuliaji kuhakikisha kuwa tunafunga mabao na kuipa ushindi timu yetu ili itwae ubingwa.

“Sijafunga katika mechi kadhaa huko nyuma, hivyo nitapambana ili nipate bao katika mchezo huu kama nitapata nafasi ya kucheza,” alisema Mavugo mwenye mabao saba katika ligi kuu.

“Nimesikia kwa miaka nenda rudi Toto imekuwa ikiifunga sana Simba lakini niseme kwamba mimi kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu tumepania sana kuifunga Toto,” alisema Mavugo raia wa Burundi.

Kabla ya hapo, Mavugo aliyejiunga na Simba akitokea Vital'O ya Burundi ndiye alikuwa chachu katika ufungaji katika kikosi cha Simba.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic