June 21, 2017

DANI ALVES (KULIA) AKISAINI JEZI ALIYOKUWA NAYO SALEHJEMBE. HAPA ALIKUWA WAKATI AKIKIPIGA BARCELONA YA HISPANIA.


Dani Alves ameamua kuvunja mkataba wake na Juventus.

Mazungumzo kati ya Alves na uongozi wa Juventus yameanza na ndani ya siku mbili tatu mwafaka utafikiwa lakini beki huyo anachotaka ni kuvunja mkataba.


Uamuzi wake huo imefahamika ni kwa kuwa ameamua kwenda kucheza soka nchini England.

Atajiunga na Manchester City inayofundishwa na boss wake wa zamani Pep Guaediola.

Alves raia wa Brazil mwenye miaka 34, walifanya kazi kwa mafanikio makubwa na Guardiola wakiwa katika kikosi cha Barcelona.


Sasa wamekubaliana kufanya kazi pamoja. Guardiola anaonekana amepania kubeba ubingwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic