June 19, 2017






Wakati kesho Jumanne Juni 20, 2017 itakuwa mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), wagombea 62 tayari wamejitokeza.
Wanafamilia hao ni wale waliojitokeza kuanzia Ijumaa iliyopita Juni 16, mwaka huu wakiongozwa na Jamal Malinzi aliyekuwa wa kwanza kuchukua fimu kati ya wagombea tisa walioomba nafasi hiyo.
Fomu hizo zinachukuliwa na kurejeshwa katika ofisi za TTF, Karume jijini Dar es Salaam na Uchaguzi wa TFF utakafanyika Agosti 12, mwaka huu mkoani Dodoma.
Mbali ya Malinzi, wengine waliochukua fomu hizo ni Imani Madega, Wallace Karia, Fredrick Masolwa, Athumani Nyamlani, Fredrick Mwakalebela na Ally Mayay wakati waliojitokeza kuwania Makamu wa Rais wako Mulamu Nghambi, Michael Wambura, Geofrey Nyange, Mtemi Ramadhani na Robert Selasela.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa kufuata Kanda 13 ni kama ifuatavyo:
Kanda Na. 1 Mikoa ya Kagera na Geita;
Soloum Chama
Kaliro Samson
Samwel Daniel
Leopold Mukebezi
Abdallah Mussa

Kanda Na. 2 Mikoa ya Mara na Mwanza;
Vedastus Lufano
Ephraim Majinge

Kanda Na. 3 Mikoa ya Shinyanga na Simiyu;
Benista Rugora
Mbasha Matutu
Stanslaus Nyongo

Kanda Na. 4 Mikoa ya Arusha na Manyara;
Omari Walii
Sarah Chao
Peter Temu

Kanda Na. 5 Mikoa ya Kigoma na Tabora;
John Kadutu
Issa Bukuku
Abubakar Zebo

Kanda Na. 6 Mikoa ya Katavi na Rukwa;
Kenneth Pesambili
Baraka Mazengo

Kanda Na. 7 Mikoa ya Mbeya na Iringa;
Elias Mwanjala
Cyprian Kuyava
Erick Ambakisye

Kanda Na. 8 Mikoa ya Njombe na Ruvuma;
James Mhagama
Golden Sanga
Vicent Majili

Kanda Na. 9 Lindi na Mtwara;
Athuman Kambi
Dunstan Mkundi

Kanda Na. 10 Mikoa ya Dodoma na Singida; 
Hussein Mwamba
Mohamed Aden
Musa Sima
Stewart Masima 
Ally Suru

Kanda Na. 11 Mikoa ya Pwani na Morogoro;
Charles Mwakambaya
Gabriel Makwawe
Francis Ndulane 

Kanda ya 12. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga
Khalid Mohamed
Goodluck Moshi

Kanda Na. 13 Mkoa wa Dar es Salaam
Emmanuel Ashery
Ayoub Nyenzi
Saleh Alawi
Shaffih Dauda
Thabit Kandoro
Abdul Sauko
Peter Mhinzi
Ally Kamtande
Said Tully
Mussa Kisoky
Lameck Nyambaya
Ramadhani Nassib

Aziz Khalfan

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic