July 6, 2017





Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA), Ramadhani Mambosasa ametoa wito wa walimu wa soka kujitokeza kwa wingi kuchukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi - ngazi ya taifa.

Mambosasa ametoa wito huo ikiwa zimebaki siku mbili tu kwa mujibu wa kanuni kukamilisha hatua hiyo. Fomu hizo zinazopatikana ofisi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam, zilianza kutolewa juzi Julai 3, 2017 na mwisho ni Julai 7, mwaka huu.

“Wanaojitokeza wachache. Wengine wanadai hawafahamu zilizo ofisi za DRFA. Tunatoa wito wajitokeze kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali,” amesema Mambosasa.


Nafasi zilizotangazwa kuwaniwa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mweka Hazina ambao fomu zao zinapatikana kwa Sh 200,000 wakati nafasi za wajumbe wa Mkutano Mkuu TFF na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji fomu zao zinapatikana kwa Sh 100,000.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic