July 6, 2017



Uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu kwa Wanawake (TWFA), sasa utafanyika Dar es Salaam badala ya Dodoma na Morogoro - mikoa iliyotangazwa awali.

Mwenyekiti Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Msomi Wakili George Mushumba, amesema kwamba taratibu zote zimekamilika na kwamba siku ya uchaguzi ni Jumamosi Julai 8, mwaka huu.

Wakili Mushumba ametoa wito kwa wajumbe wote kufika Dar es Salaam Ijumaa Julai 7, mwaka huu kwa ajili ya kufahamu tararibu za awali za uchaguzi.

Tayari Kamati ya Mushumba ilitangaza majina ya wagombea 11 waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu.

Majina ambayo yamepitishwa ni Amina Karuma, Rose Kisiwa, Somoe Ng’itu, Theresia Mung’ong’o, Hilda Masanche, Salma Wajeso, Zena Chande, Triphonia Temba, Mwamvita Kiyogoma, Jasmine Soudy na Chichi Mwidege.


Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mweka Hazina, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na Wajumbe wanne wa Kamati ya Utendaji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic