July 2, 2017


Taifa Stars imetinga nusu fainali ya michuano ya Cosafa baada ya kuwatwanga wenyeji Afrika Kusini kwa bao 1-0.

Shuja wa mechi hiyo ambaye ameibuka nyota wa mchezo huo amekuwa ni Elius Maguri ambaye amefunga bao hilo pekee katika kipindi cha kwanza.

Kipa Aishi Manula mara kadhaa alilazimika kuokoa michomo mikali ya washambuliaji wa Afrika Kusini.

Safu ya ulinzi iliyoongozwa na Erasto Nyoni na Salim Mbonde ilionekana kukaa imara tokea kipindi cha kwanza lakini Muzamiru Yassin na Raphael Alpha wakaonekana kufanya vizuri zaidi katika.

Simon Msuva aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Thomas Ulimwengu na kusaidia kuongeza nguvu ya kupandisha presha kwenye lango la Afrika Kusini.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic