August 13, 2017



Madrid, Hispania
KOCHA wa Real Madrid, Zinedine Zidane, amesema anafuraha kubwa kusaini mkataba wa kuendelea kuifundisha timu hiyo, lakini haimaanishi kuwa atakaa hapo kwa muda mrefu.

Zidane ambaye amekuwa na mafanikio makubwa sana kwenye timu hiyo akiwa ameshatwaa ubingwa wa La Liga na Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili, amesaini mkataba wa miaka mitatu na timu hiyo.

Baada ya kusaini, kocha huyo raia wa Ufaransa amesema urefu wa mkataba huo hauna maana yoyote kama timu hiyo itakuwa haifanyi vizuri uwanjani, inamaanisha kuwa ataondoka hapo.

“Habari yangu na Real Madrid ni kubwa kuliko inavyofikiriwa, lakini hapa pana historia pana kuliko kusaini mkataba na timu hii.

“Nafurahia kusaini mkataba na klabu hii, lakini haimaanishi kuwa nitakuwa hapa kwa kipindi chote cha miaka mitatu.

“Nafahamu hapa nilipo, unaweza kusaini mkataba wa miaka kumi au 20, lakini usikae hapo zaidi ya mwaka mmoja. Kama sitafanikiwa nitaondoka hapa na Madrid hawawezi kulalamika,” alisema Zidane.

Zidane alikabidhiwa timu hiyo mwaka 2016, baada ya kuondoka aliyekuwa kocha wa timu hiyo Rafael Benitez na tayari ameshatwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili na La Liga mara moja.

Pia ameiwezesha Madrid kutwaa Ubingwa wa Klabu Bingwa Dunia mara moja na Kombe la Uefa Super Cup, alipowafunga Manchester United mabao 2-1 wiki iliyopita.

1 COMMENTS:

  1. Super payer, super coach... Kazi kwetu watz. Ninmwndo wa makinikia mpaka kwenye soka...

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic