Mechi ya upinzani mkubwa jijini Istambul kati ya Fenerbahce dhidi ya Besiktas imeweka rekodi mpya baada ya wachezaji watano kulambwa kadi nyekundu.
Mechi hiyo iliyochezwa leo iliisha kwa Fenernahce kushinda kwa mabao 2-1 lakini kadi 11 za njano zilitembea.
Wachezaji watano wa timu hizo walitolewa nje huku watatu kati ya hao wakitolewa nje katika dakika 5 za mwisho.
Wachezaji waliolambwa kadi nyekundu katika Uwanja wa Ulker ilipochezwa mechi hiyo ni pamoja na Ricardo Quaresma, Luis Neto, Atiba Hutchinson, Ismail Koybasi na Oguzhan Ozyakup.
0 COMMENTS:
Post a Comment