October 27, 2017


Kikosi cha Simba kinatarajia kurejea jijini Dar es Salaam leo kwa maandalizi ya mwisho ya mechi yao ya kesho dhidi ya Yanga.

Simba walikuwa kambini mjini Zanzibar kujiandaa na mechi ya Ligi Kuu Bara itakayopigwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Taarifa zinaeleza, Simba watawasili kwa kutumia ndege za kukodi tayari kwa ajili ya mechi hiyo.

Kikosi hicho kitaingia kambini jijini Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi ya mwisho.


Hata hivyo, Simba wamekuwa wakifanya uficho kuhusiana na sehemu watakayokaa jijini Dar es Salaam wakimalizia maandalizi yao hayo ya mwisho kabla ya kesho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic