November 2, 2017

TIMU ya Simba inatarajiwa kusafiri kesho Ijumaa saa tatu kamili asubuhi kwa njia ya ndege kuwafuata wapinzani wao Mbeya City kwa ndege.

Simba itaelekea mkoani Mbeya kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu Bara itakayopigwa Jumapili ya wiki hii kwenye Uwanja wa Sokoine mkoani huko.

Katika mechi hiyo, Simba itavaana na Mbeya ikiwa na hasira ya kuzikosa pointi tatu za mechi iliyopita dhidi ya Yanga.

Akizungumza na Salehjembe, Mratibu wa timu hiyo, Abbas Ally alisema taratibu zote za kukamirisha safari hiyo zimekamilika.

“Timu inatarajiwa kuondoka jijini Dar kesho saa tatu kamili asubuhi na ndege tukielekea Mbeya kwa ajili ya mchezo wetu wa Jumapili dhidi ya Mbeya City.
“Tutakuwa tukiwa hatuna majeruhi yeyote katika kikosi chetu, hivyo ni jambo jema kwetu katika kufanikisha pointi tatu katika mchezo wetu huu muhimu,”alisema Ally

1 COMMENTS:

  1. ������ nimekutana na basi la simba iringa likiwa linaelekea mbeya

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic