Mshambuliaji Obrey Chirwa anatarajia kuanza mazoezi kesho asubuhi akiungana na wenzake akiwa gym.
Pamoja na Chirwa kuanza mazoezi, kiungo Papy Tshishimbi naye anatarajia kuanza mazoezi leo.
Tshishimbi naye alisimama kufanya mazoezi kutokana na kusumbuliwa na majeraha.
Wote wawili wataanza mazoezi na wenzao wakati Yanga itakapokuwa inaanza mazoezi baada ya mapumziko ya siku mbili.
Mazoezi ya kesho Jumapili yanatarajia kuwa yale ya gym na Jumanne, Yanga wataanza mazoezi ya uwanjani kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu Bara.
0 COMMENTS:
Post a Comment