December 17, 2017




Kocha Jurgen Klopp wa Liverpool amefunguka kwamba aliingia hofu kumsajili Mohamed Salah hadi alipigwa presha.

Klopp amesema kitengo cha kusaka wachezaji cha Liverpool kilimpa presha kutaka Salah asajiliwe jambo ambalo alikuwa hakubaliani halo kwa hofu ya jumbo dogo la Salah.

Kocha huyo Mjerumani amesema, aliamini kwa jumbo la Salah kulikuwa na hofu ya kufanya vizuri Ligi Kuu England.

Wakati huo, wachezaji wake watatu ambao ni Philippe Coutinho, Sadio Mane na Roberto Firmino, aliamini wangebadilika na kumbeba.

Baadaye alikubali na Liverpool iliilipa AS Roma kitita cha pauni million 34 hali ambayo pia ilizua mjadala.

Lakini tayari Salah ametupia mabao 19 katika michuano tote akiwa na Liverpool na sasa winga huyo anaonekana ni tegemeo.

Salah ambaye ni mchezaji bora wa Afrika kupitia BBC ndiye anayeongoza kwa upachikaji wa mabao katika Ligi Kuu England akiwa na mabao13.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic