December 27, 2017


Beki na kiungo kiraka mpya wa Simba, Asante Kwasi rasmi ameanza mazoezi akiwa na uzi wa klabu hiyo.

Kwasi aliyewasili jijini Dar es Salaam, jana jioni akitokea Iringa, ameanza mazoezi kwenye ufukwe wa Coco.

Raia huyo wa Ghana ndiye alikuwa gumzo zaidi wakati Simba ikifanya juhudi za kumsajili na Lipuli FC wakipinga.

Hata hivyo, baadaye timu hizo zilifikia mwafaka na mwisho Kwasi sasa ni mali ya Simba.

Hata hivyo, ili awe mali ya Simba mchezaji huyo ilikuwa ni lazima aonekane katika uzi wa Simba na si ule wa Lipuli ambao wengi walikuwa wakiufananisha na wa Simba.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic