December 20, 2017




Kamati ya Usajili ya Simba, imetangaza kumbakiza kundini mshambuliaji wake Laudit Mavugo raia wa Burundi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema baada ya kumtema beki Method Mwanjale, hawana mpango wa kumuacha mchezaji mwingine.

Hans Poppe amesema Simba haina mpango wa kumuacha mchezaji licha ya kuelezwa kwamba Mavugo analazimika kumpisha Dayo Domingues kutoka Msumbiji.


“Hatuna mpango wa kumuacha mtu yoyote baada ya Mwanjali, hivyo baada ya usajili wa Kwasi kukamilika, hatutakuwa na usajili mwingine,” alisema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic