Pierre-Emerick Aubameyang ameonekana uwanja wa ndege wa Luton nchini Ujerumani akijiandaa kupanda ndege ya kukodi.
Taarifa zimeeleza anakwenda London, England kumalizana na Arsenal katika like dili lake la pauni million 55 akitokea Borussia Dortmund.
Aubameyanga ameonekana akishuka kwenye gari aina ya Range Rover akiwa na baba yake mzazi Pierre na wadogo zake Catilina na Willy na imeelezwa kwamba wanamsindikiza London.
Hali ilivyo inaonekana kama ni uhakika kwa kuwa tayari kuna baadhi ya sehemu jezi za Aubameyang za Arsenal zenye namba 14 zimeanza kuuzwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment