January 20, 2018


Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma bado ni majeruhi na hajajiunga na wenzake.

Lakini jana aliamua kuwatembelea wenzake mazoezini kwenye Uwanja wa Uhuru wakati wakiendelea kujifua kujiandaa na mechi za Ligi Kuu Bara.


Raia huyo wa Zimbabwe, ameendelea kukaa nje kwa zaidi ya miezi miwili sasa na imekuwa zaidi ya wiki tatu tokea arejee Dar es Salaam akitokea kwao Zimbabwe ambako ilielezwa amekwenda kupata matibabu nchini Afrika Kusini.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic