Mkongwe aliyewahi kuichezea Liverpool, Jammie Carragher, ameomba radhi kutokana na kitendo cha kumtemea mate binti mwenye miaka 14 ambaye ni shabiki wa Manchester United.
Carragher alionekana akimtemea mate binti huyo aliyekuwa kwenye gari na baba yake, ikiwa ni mapema baada ya mechi iliyowakutanisha Manchester United na Liverpool Jumamosi iliyopita.
Binti huyo alimtania Carragher kuhusiana na matokeo ambayo Liverpool alifungwa 2-1, jambo lililosababisha mkongwe huyo kupandwa na hasira.
Carragher ambaye ni Mchambuzi kwenye kituo cha Sky Sports TV, alimpigia msichana huyo Jumapili ya jana kumuomba msamaha kwa kitendo alichokifanya na binti huyo alipokea msamaha wake.
Kwa mujibu wa Sky Sports TV, Msemaji wa Chombo hicho amesema kitendo alichokifanya Carragher si cha kuchukuliwa kawaida, hivyo watakutana naye na ikiwezekana watachukua hatua dhidi yake.









0 COMMENTS:
Post a Comment