March 11, 2018


Inawezekana ikawa pengo kubwa kwa Tottenham Hotspurs baada ya Mshambuliaji wake hatari, Harry Kane, kuumia leo katika mchezo wa ligi dhidi ya Bournemouth.

Tottenham imeibuka na ushindi wa mabao 4-1, matokeo ambayo yameifanya timu hiyo ipande mpaka nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi.

Kane alitolewa dakika ya 30 ya kipindi cha kwanza baada ya kugongana na kipa wa Bournemouth, Asmir Begovic, na kupelekea kuumia enka ya mguu wa kulia.

Kufuatia tukio hilo, Kane alitolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Erik Lamela.

Kocha wa Tottenham, Mauricio Pochettino, amesemakuwa anadhani hajaumia japo itabidi wasubiri majibu kutoka kwa daktari.

Kane ameumia huku klabu yake ikiwa katika maandalizi ya kucheza na Swansea City kwenye Kombe la FA, vilevile timu yake ya taifa, England itakipiga dhidi ya Netherlands Ijumaa ya wiki litakalofuata, Machi 23 2018. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic