March 13, 2018


Klabu ya Al Masry imelazimishwa suluhu ya 0-0 dhidi ya El Entag El Harby katika mchezo wa Ligi Kuu Misri uliopigwa jana.

Al Masry wamelazimishwa suluhu hiyo wakiwa wanajiandaa kuwakabili vinara wa Ligi Kuu Bara, Simba SC, Jumamosi ya wiki hii kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Africa.

Kuelekea mechi hiyo, Al Masry sasa ipo nafasi ya 4 katika msimamo wa Ligi Kuu nchini humo ikiwa na pointi 49 wakiwa wamecheza michezo 26.

Mechi yao dhidi ya Simba itafanyika Machi 17 2018 kwenye Uwanja wa Port Said Jumamosi ya wiki hii.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic