April 19, 2018



Kikosi cha Yanga kinatarajia kuwasili nchini majira ya saa saba usiku kikitokea Ethiopia kushiriki mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika majira dhidi ya Wolaita Dicha SC.

Yanga ilifanikiwa kusonga mbele na kuingia hatua ya makundi kwa jumla ya mabao 2-1 ambao jana ilipoteza kwa bao moja.

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Dar es Salaam Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 na kutengeneza mazingira ya mchezo wa marudiano uliopigwa jana Awassa, Ethiopia.

Baada ya kuwasili nchini, Yanga itatakiwa kusafiri kuelekea Mbeya, kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbeya City FC.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic