April 2, 2018



Na George Mganga

Kikosi cha Simba kimeondoka mjini Iringa asubuhi ya leo kuelekea Njombe kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Simba imeondoka Iringa baada ya kambi maalum ya muda mfupi ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi dhidi ya Njombe Mji FC.

Mchezo huo utapigwa kesho Uwanja wa Sabasaba mjini humo kuanzia saa 10 kamili jioni.

Kuelekea mchezo huo, hali ya Kiungo, Jonas Mkude , inaendelea vizuri kwa sasa kutokana na kuanza mazoezi mepesi jana Jumapili.

Mkude aliumia wakati Simba ikiwa jijini Dar es Salaam, Jumatatu ya wiki iliyopita kwenye mazoezi yaliyofanyika Uwanja wa Boko Vetarani baada ya kukwaana na Mzamiru Yassin.

Mkude alianza mazoezi mepesi jana chini ya uangalizi wa Daktari wa timu, Yassin Gembe, na taarifa zinaelezwa kuwa hali yake inazidi kuimarika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic