April 30, 2018



Kiungo wa klabu ya Simba Jonas Mkude jana amechagukiwa kuwa mchezaji bora wa mechi katika timu yake, na hii ni kwa mujibu wa kura zilizopigwa na mashabiki kupitia kurasa za mitandao ya kijamii.

Mkude alitangazwa kushinda nafasi hiyo mapema baada ya mchezo dhidi ya Yanga kumalizika kwenye Uwanja wa Taifa jana ambapo Simba walifanikiwa kushinda kwa bao 1-0.

Mbali na kuchagulia na mashabiki, mchezaji wa zamani wa Yanga, Sekilojo Chambua, ameeleza kuwa Mkude ndiye mchezaji bora pia kwake, kutokana na namna ambavyo alicheza jana Uwanjani.

Chambua amesema kuwa Mkude alikuwa akitengeneza mipira mizuri katikati mwa Uwanja na kuwalisha wenzake, huku akishindwa kuipoteza bali aliihimili vizuri.

Chambua amempa nafasi ya ubora Mkude katika mchezo baada ya kuiongoza safu ya kiungo vizuri na kuifanya iwe bora zaidi dhidi ya watani zao Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic