April 9, 2018



Baada ya mchezo wa ligi kati ya Mbeya City na Azam FC kwenda suluhu ya bila kufungana katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, uongozi wa Azam waitupiwa lawama Mbeya City.

Kupitia Afisa Habari wa Azam, Jaffer Idd Maganga, alisema kuwa wachezaji wa Mbeya hawakuwa wanacheza mpira kupata matokeo bali walipambania pointi moja.

Maganga alieleza kuwa wapinzani wao walikuwa wanatumia muda mwingi kupoteza muda huku akieleza kuwa walikuwa wameridhika ilihali wao walikuwa wanapambana kujipatia alama 3 muhimu.

Azam iliambulia alama moja kwenye mchezo na kuzidi kusalia katika nafasi ya 3 ya msimamo wa ligi kuu bara ikiwa na pointi 45 huku ikicheza jumla ya michezo 23 mpaka sasa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic