April 3, 2018



Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Young Africans, wameweka tena kambi nyingine maalum mjini Morogoro kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Welayta Dicha FC.

Yanga ilitua Morogoro jana ikitokea mkoani Singida kucheza mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Singida United kwenye hatua ya robo fainali ambapo iliondolewa kwa changamoto ya mikwaju ya penati (4-2).

Kikosi hicho kimeshindwa kufika Dar es Salaam na kuamua kuishia Morogoro kwa ajili ya mawindo dhidi ya Welayta Dicha FC kutoka Ehtiopia inayotaraji kuwasili nchini wiki hii.

Yanga itacheza na Waethiopia hao Jumamosi ya Aprili 7 2018 katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, kabla ya kurudiana nao huko Ethiopia baada ya wiki moja mbele.


1 COMMENTS:

  1. Bora mjipe moyo manaake mambo hatarihatari

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic