Nyota inaendelea kumuwakia beki kiraka wa Simba, Shomari Kapombe kwani sasa taarifa zinasema anatakiwa na moja ya timu iliyopanda kucheza Ligi Kuu ya Hispania msimu ujao.
La Liga ni ligi kubwa Ulaya ambapo mastaa mbalimbali wanacheza wakiwemo Lionel Messi wa Barcelona na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid.
Chanzo cha habari kutoka ndani ya Simba, kimeeleza kuwa timu kubwa kutoka Hispania ambayo imepanda ligi kuu inamtaka Kapombe alipokuwa akiichezea Simba mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Masry ya Misri baada ya kuvutiwa na uwezo wake.
Kwa mujibu wa gazeti la Championi lilimtafuta Kapombe ili aweke wazi kuhusiana na taarifa hizo, ambapo alisema: “Nikweli kuna mawakala zaidi ya watatu wamenipigia hivi karibuni wakinitaarifu uwepo wa timu zaidi ya tatu kunihitaji.”
“Wakala wa kwanza ameniambia kuna timu ya Hispania inanitaka, lakini pia zipo zingine mbili, moja kutoka Urusi na nyingine ipo Bara la Asia ambazo zote nimeshataarifiwa kunihitaji, hivyo wakala wangu ameniomba nitume tu baadhi ya ‘clip’ (video) zangu ili aweze kukamilisha dili hilo.
“Hii ni bahati sana kwangu kuonekana kwa muda mfupi huu ambao nimecheza Simba, japo nia yangu ningependa kuendelea kuwa hapa ili nijiweke vizuri zaidi kwani nina malengo mengi sana ambayo bado sijayafikia pamoja na kwamba wao wameshaona uwezo wangu,” alisema Kapombe.
Safi sana kapombe. Siku zote kizuri hujiuza tu wala hakihitaji makelele kukinadi. Kwa tunavyomfahamu kapombe kama atakuwa fiti akikanyaga Spain tu, ukisikia yupo Real Madrid sio jambo la kushangaza ni kijana mwenye nizamu,kujituma na adabu ya kutosha. La Msingi kutoka kwa viongozi wake wa SIMBA wajarbu kumuekwa mazingira rahisi ya kutua Spain kuliko hizo sehemu nyengine.
ReplyDeleteunastahili
ReplyDeleteunastahili
ReplyDeleteDahh huyu jamaa ana bahati sana na Simba,
ReplyDeleteWale wa Sunderland walishaenda ? Bongofix
ReplyDeleteSimba imekuwa daima chimbuko la nyota wanaogombaniwa ughaibuni kuliko timu zote za nyumbani na imekuwa ikiwabariki wachezaji hao kila inapotokea fursa kama jizo kwenda kujipatia riziki zao bila ya kinyongo baadya kuwalea na kuwatakia kila la heri bila ya kinyongo
ReplyDelete