May 25, 2018





Mshambuliaji Sadio Mane amenunua jezi 300 na kuzituma kijijini kwao nchini Senegal.
Jezi hizo za Liverpool zitavaliwa kesho wakati Liverpool ikiivaa Madrid katika mechi ya fainali ya Ligi ya Mabingwa jijini Kiev.

Mane amesema amefanya hivyo baada ya kusikia katika kijiji alichozaliwa cha Bambali, kuna watu wengi wameamua kuhama timu kadhaa na kuiunga mkono Liverpool kesho.

Mane amekumbusha kwa kusema hata yeye, aliwahi kuwa shabiki mkubwa wa FC Barcelona kabla ya kuhamishia mapenzi yake Liverpool.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic